Moto unaowashwa na chipukizi wa Liverpool aliyepo kwa mkopo katika klabu ya Hull City inayoshiriki ligi daraja la kwanza maarufu kama champi...
Moto unaowashwa na chipukizi wa Liverpool aliyepo kwa mkopo katika klabu ya Hull City inayoshiriki ligi daraja la kwanza maarufu kama championship, Harry Wilson umepelekea timu hiyo kuhitaji zaidi huduma yake.
Kocha wa Hull, Nigel Adkins ameripotiwa akisema kuwa anatamani kuendelea kuwa na nyota huyo ambaye alijiunga na kikosi chake katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari mwaka huu.
" Ni mchezaji mzuri ambaye maendeleo yake yamekuwa makubwa kwa kipindi cha muda mfupi tuliokaa nae hapa, bado ana mengi ya kujifunza na kukua zaidi licha ya kuwa bado ni mchezaji kinda lakini amekuwa msaada kwetu katika kila mchezo tunaocheza, bado natamani kuendelea kuwa nae," amefichua Kocha Adkins.
Wilson amekuwa na takwimu zenye kuvutia ndani ya kikosi cha Hull ambapo amecheza michezo 11 mpaka sasa na kutupia nyavuni magoli matano huku akisaidia upatikanaji wa mengine manne.
Kocha wa Hull, Nigel Adkins ameripotiwa akisema kuwa anatamani kuendelea kuwa na nyota huyo ambaye alijiunga na kikosi chake katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari mwaka huu.
" Ni mchezaji mzuri ambaye maendeleo yake yamekuwa makubwa kwa kipindi cha muda mfupi tuliokaa nae hapa, bado ana mengi ya kujifunza na kukua zaidi licha ya kuwa bado ni mchezaji kinda lakini amekuwa msaada kwetu katika kila mchezo tunaocheza, bado natamani kuendelea kuwa nae," amefichua Kocha Adkins.
Wilson amekuwa na takwimu zenye kuvutia ndani ya kikosi cha Hull ambapo amecheza michezo 11 mpaka sasa na kutupia nyavuni magoli matano huku akisaidia upatikanaji wa mengine manne.


COMMENTS